Wanangu niaje?
Nimekula misaim ya kutosha judoka kwa sana kitaani wananimaindi nimechelewesha kupandisha Zee la wiki hii hewani, hivi wanangu si nilisema Jumatatu? Kwani niliwaambia na taimu? Sasa mbona mnaanza kukoroma bado mapema? Au ndio Kiu ya ishu za tauni? Msikonde basi nishamalizana nayo hii hapa ishu ya wiki hii inadondoka kama kawa.
Ujue bwana, tauni miyeyusho sana samtaimz, na ndio maana last wiki nikawa nawaambia madogo kama vipi vileji kunawahusu, hizi laifu za kufosi hizi, kuna watu zinawakosti sana, ingawa wenyewe wanaona kama poa hivi, ila sio poa wala nini, miyeyusho tu mwanangu mwenyewe.
Sasa kund yanki flani vivi saundi sana hapa tauni, mwenyewe huwa akiniona ananichukulia poa sana kumbe mtu mzima na mimi miyeyusho kitambo sana, ila kwa sababu nshakuwa zee kweli, nimeamua kukausha na kudili na ishu zilizonyooka. Haya mambo ya saundi nimeamua kuwaachia magumashi junia.
Umeona bwana?
Sasa Jamal juzikati kanijia na mchongo wake wa madini, unaona bwana? Unajua ananipa zipi? Kuna chili wake autoka Naijeria alikuja kumtembelea, akagundua kwamba shambani kwa mshua wake Kuna ishu, lakini wanatafuta mtu mwenye jina tauni ili wakachukue mkopo samwea waanze kutemesha mzigo.
Umeskia mwanangu?
Nikamuuliza mean, h\ishu yenyewe Kiko mkoa gani? Mwana bila noma wala nini akanichana kwamba ishu Dar hii hii ila Mkuranga flani hivi mshua wake anapiga ishu za matikiti. Sasa huyo mana latina misele yace amaina dizaini flani za mchanga ambo sio wa kawaida.
…machale yakanidensi….
Madini Mkuranga? Waeniona boya kiasi gani Hawa mayanki, ila nikajifanya kama Boya kweli, na mimi nikamtuliza, nikamwambia mwanangu sio ishu, ila sasa inabidi wataalam wazuke pale shamba wakapige risechi mbili tatu ili hata huko samwea tukienda kuchukua mkopo, tupeleke dokumenti zinazowapa uhakika washua kwamba mzigo upo.
Umenisoma babu?
Nikamwambia na gharama za ndani, yaani za risechi na nini inabidi mimi mwenye jina kwa sababu ndio nitakayezama kitaa kwenda kutafuta mkopo nipewe ili nikalete watu wa uhakika, niwalipe ili Kazi ianze. Umeona mwanangu mwenyewe? Hapo nikawa nishamgeuzia kibao kama alitaka anitemeshe mzigo ikawa inabidi auteme yeye sasa.
Mwana akanichekiiii, na mimi nikawa nimemkazia uso, uso wa Kazi ile ile nikamwambia ndio hivyo, mie nina wanangu akina Le Mutuz wana koneksheni tauni lakini wanataka vitu vilivyonyooka ili na way wanyooshe dili kama kweli zipo.
Akajikata, huku nyuma sasa ndio nikabaki na maswali, huyu mchizi mimi kanichukuliaje? Madini Mkuranga? Hivi kuna watu mpaka leo mnafkiri tauni kuna washamba? Sawa wanaweza kuwepo, ndio mimi sasa Zee mwenyewe?
Ndio maana mnasema maisha magumu kudadadeki kumbe mpaka fiksi zimewaishia, na huu ndio mwisho wa miyeyusho kudadadeki, ukiona aidia za manage zinakuishia ujue mwanangu unatakiwa kuachana nazo na kurudi kwenye ishu za kunyoosha.
Sasa bora umekutana na Zee, anakubananisha na ishu, mwingine anakupa mkwanja ila ukimletea miyeyusho anakurudisha kijijini kwa kichapo, unafilisiwa kwanza, unakula kichapo, jela miaka kadhaa halafu vileji.
Kipi bora?
Jiangalie plaza